Wednesday, May 7, 2014

ZILE tuzo saba alizotwaa nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ kwenye mkesha wa Jumapili iliyopita ndani ya Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam zimezua balaa! Ni balaa gani hilo? Risasi Jumatano linakumegea.
Msanii Diamond Platnumz akipozi na tuzo zake.
Kwa mujibu wa chanzo makini, baadhi ya ndugu wa Diamond walicharuka kufuatia staa huyo aliyeshinda nafasi ya Msanii Bora wa Kiume wa Bongo Fleva 2014, kuzibeba tuzo hizo na kwenda kulala nazo kwa Wema Sepetu anayemtaja kuwa ni mpenzi wake kwa sasa.
Diamond na mama yake wakipozi na tuzo.
MANENOMANENO YA BAADHI YA NDUGU
“Unajua kilichowakwaza sana baadhi ya ndugu ni kitendo cha Diamond kwenda kulala kwa Wema, Kijitonyama na tuzo zote saba.
“Wanasema alichotakiwa kukifanya, mara baada ya kutoka ukumbini angekwenda nazo nyumbani kwao (Sinza-Mori) akaziacha kisha ndiyo aende kwa huyo Wema wake,” kilisema chanzo hicho.
Kikaongeza:
...Akipokea tuzo kutoka kwa George Kavishe.
“Ujue Diamond anakoelekea anaanza kupotoka kwani mwanzo alikuwa haachani na mama yake hasa kwenye ishu kubwa kama hizo, mwaka huu ameonesha utovu wa nidhamu, maana ndugu wanaamini hakutaka kwenda na mama yake ukumbini kwa sababu alijua atakuwa na Wema.”
MARAFIKI PIA WASHANGAZWA
Chanzo kiliendelea kuanika kwamba baadhi ya  marafiki wa Diamond nao walionesha kushangazwa na kitendo cha mama Diamond (Sanura Kasim) kutoonekana kwenye ukumbi wakati mwanaye akipokea tuzo badala yake nyota huyo kuwa beneti na Wema.
Diamond akipokea tuzo kutoka kwa prodyuza Tuddy Thomas.
“Baadhi ya marafiki wamesema kuna kitu, kwa vile wanavyojua wao, shoo au jambo lolote ambalo Diamond anahusika, mama yake lazima aibuke naye. Wengi wanaamini uhusiano wa mama na mwanaye umevurugwa na kitendo cha Wema kurudiana na baby wake huyo,” kilisema chanzo hicho.
Kikaendelea: “Lakini kuna watu wanadai mama Diamond siku hiyo aliamua kwenda kwenye bethidei ya mpenzi wa zamani wa Diamond, yule Penny kwa sababu alipuuza uwepo wa Wema ukumbini.”
Mama yake Diamond akiwa na mtangazaji wa DTV Penny ambaye ni mpenzi wa zamani wa Diamond.
NDUGU WASAKWA
Baada ya paparazi wetu kuzinyaka taarifa hizo, alianza kuwasaka baadhi ya ndugu hao ili kujua ukweli wa madai yote.
WA KWANZA MAMA DIAMOND
Mtu wa kwanza kupatikana kwenye familia hiyo ni mama Diamond mwenyewe ambapo alibanwa kwa maswali kadhaa kama ifuatavyo:
Paparazi: “Mama Nasibu nimekuja kwa mambo mawili matatu. Kwanza nataka kujua ni kwa nini hukuonekana ukumbini siku ya Tuzo za Kili wakati mwanao anazoa tuzo saba? Maana wengine wanasema uliogopa uwepo wa Timu Wema, wengine wanasema ulikwenda kwenye bethidei ya Penny.
Penny akiwa katika pozi.
Pia kuna minong’ono kwamba, familia imechukizwa na kitendo cha Diamond kwenda kulala na tuzo zake nyumbani kwa Wema, ni kweli?
Mama: “Kwanza kabisa, siku ile mimi sikuwa na mpango wa kwenda kwenye shughuli hiyo, hasa niliposikia itaoneshwa laivu kwenye runinga.
“Napenda kukwambia kwamba kuanzia sasa huo ndiyo utakuwa utaratibu wangu. Zamani nilikuwa nikienda kwenye shoo, hasa zinazomuhusisha Diamond  kwa vile nilikuwa sijamuona namna ya utendaji kazi wake lakini sasa namwamini anaweza kuchapa kazi hata mimi nisipokuwepo.
...akipozi na mpenzi wake wema Sepetu.
KUHUSU TIMU WEMA, BETHIDEI YA PENNY
“Wanaosema mimi sijaenda ukumbini kwa sababu eti nilikuwa nikihofia Timu Wema si kweli na wala sikwenda kwenye bethidei ya Penny kama wasemavyo.
“Ninaomba itambulike kwamba mimi siko kwenye timu yoyote ile, kama timu basi mimi nipo Wasafi (ya Diamond) kwa maana ninamsapoti mwanangu kwa kila kazi yake na wala sina kitu tofauti na hicho.”
Tuzo za Diamond.
DIAMOND SASA
Diamond naye alikutwa nyumbani kwao siku hiyo akiwa na tuzo hizo ambazo ilidaiwa alikwenda nazo asubuhi iliyofuata baada ya kuamka kwa Wema, alipoulizwa juu ya kupitiliza nazo hadi nyumbani kwa Wema badala ya kuzipeleka kwa mama yake, alionekana kushindwa kujibu zaidi ya kucheka na kusema:
“Wabongo bwana, hawakosi sababu na maneno ya kuongea kwa kila kitu hata kama ningefanya nini lazima wangepata tu kipya cha kunizungmzia hivyo kwa hilo sina hata cha kujibu ila tuzo zipo hapa nyumbani kwa mama.”
KUHUSU MAMA YAKE KUTOKWENDA UKUMBINI
“Kuhusu mama kutokwenda ukumbini mimi najua wazi kwamba hakuhitaji na aliomba aangalizie nyumbani kupitia runinga na kusema kweli nimefurahi sana kupata tuzo hizi ingawa pia furaha yangu itakuwa kubwa sana kama nitanyakua na tuzo ya Channel O,” alisema Diamond.
Nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ akipokea tuzo kutoka kwa Wema Sepetu.
HALIMA KIMWANA
Baada ya Diamond kuweka wazi, paparazi wetu alimtafuta Halima Kimwana ambaye naye alidaiwa kukacha kuzama ukumbini hapo kwa kuwa tu hana uhusiano mzuri na Wema na kwamba siku hiyo anadaiwa kwenda kwenye bethidei ya Penny ambaye ndiye rafiki yake kipenzi kwa sasa tangu alipoachika kwenye penzi la Diamond, msikilize Halima:
“Jumamosi siku tuzo zinatolewa mimi nilikuwa safarini Morogoro ambapo nilikwenda kufanya mambo yangu na mjini nilirudi Jumapili na mchana huohuo nilikwenda kweli kwenye bethidei ya Penny.
“Naomba ieleweke kwamba mimi sijakimbia timu yoyote na wala sitambui kama kuna kitu kinaitwa Timu Wema ila najua tu kaka Diamond ana uhusiano na Wema Sepetu, sijui hiyo Timu Wema ndiyo chombo gani?
cdt: GPL

0 comments:

Post a Comment